Psalms 61

Kuomba Ulinzi

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Nyuzi Za Uimbaji. Zaburi Ya Daudi)


1 aEe Mungu, sikia kilio changu,
usikilize maombi yangu.


2 bKutoka miisho ya dunia ninakuita,
ninaita huku moyo wangu unadhoofika;
uniongoze kwenye mwamba
ule ulio juu kuliko mimi.

3 cKwa kuwa umekuwa kimbilio langu,
ngome imara dhidi ya adui.


4 dNatamani kukaa hemani mwako milele,
na kukimbilia chini ya uvuli wa mbawa zako.

5 eEe Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu,
umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.


6 fMwongezee mfalme siku za maisha yake,
miaka yake kwa vizazi vingi.

7 gYeye na atawazwe kwenye kiti cha enzi mbele za Mungu milele;
amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.


8 hNdipo daima nitaliimbia sifa jina lako
na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.
Copyright information for SwhKC